BASHUNGWA AWASILI WILAYANI MAFIA KWA ZIARA YA KIKAZI
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa (Mb) amewasili wilayani Mafia mkoani Pwani kufanya ziara ya kikazi ambapo amepokelewa na Mkuu wa Wilaya ya Mafia, Aziza Mangosongo, leo tarehe 22 Machi 2024. Bashungwa amepokelewa pia na Mbunge wa Mafia ambaye pia ni Naibu Waziri wa Elimu, Omary Kipanga pamoja na viongozi wa Serikali na Chama Cha Mapinduzi. […]