Home > Articles posted by MACHINGA TV (Page 144)
FEATURE
on Dec 28, 2023
249 views 6 mins

Na Happiness Shayo Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) amesema Tamasha la Kilimanjaro Cultural Festival linalohusisha utamaduni wa vyakula ,ngoma na lugha za asili za jamii ya Wachaga, Wapare na Wamaasai litasaidia kukuza utalii wa Mkoani Kilimanjaro endapo litaendelezwa na kutumika ipasavyo. Amesema lengo la Tamasha hilo ni kukuza na kuhamasisha utalii […]

FEATURE
on Dec 28, 2023
271 views 4 mins

*Mashine Mbili za Megawati 47O zimeshafungwa, majaribio yameanza* *Ujazo wa maji watosha kuanza kuzalisha umeme* *Dkt. Biteko asema kipaumbele ni upatikanaji wa umeme wa uhakika nchini* Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa, utekelezaji wa  mradi wa umeme wa Julius Nyerere (JNHPP) utakaozalisha megawati 2,115 kwa sasa umefikia asilimia […]

FEATURE
on Dec 28, 2023
248 views 2 mins

Awaomba kuendela kutoa ushauri mzuri na kutoa miongozi itakayowasaidia Viongozi wa Chama na Serikali kuendelea kuwatumikia Watanzania kwa misingi ya Haki._ Katibu wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (NEC), Idara ya Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Ndugu Paul Christian Makonda, amewashukuru na kuwaomba Viongozi wote wa Dini nchini, kudumisha ushirikiano kwa viongozi wa Chama na […]

FEATURE
on Dec 28, 2023
349 views 17 secs

Na, Brown Jonas – WUSM Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi ameridhia ushauri wa kuubadili jina uwanja wa Amaan na kuitwa “New Amaan Sports Complex” wakati wa uzinduzi wa awamu ya tatu ya Uwanja huo uliofanyika Desemba 27, 20203 kisiwani humo Rais Mwinyi ameridhia ushauri huo uliotolewa […]

FEATURE
on Dec 27, 2023
401 views 9 secs

Na Mwandishi wetu.Babati HABARI Mahakama ya wilaya ya Babati imeifutilia mbali kesi ya ukatili iliyokuwa inamkabili mbunge wa jimbo la Babati Mjini, Pauline Gekul kuhusu tuhuma za unyanyasaji kwa kijana Hashim Ally. Uamuzi huo umetolewa leo Desemba 27, 2023, na Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya wilaya Babati, Victor Kimario na kusema ameifuta baada ya Mkurugenzi […]

FEATURE
on Dec 27, 2023
469 views 4 mins

MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ya Tanzania (DCEA) imekatama kilogramu 3,182 za dawa za kulevya aina ya heroin na methamphetamine ambazo zilikuwa zimefungashwa kwenye vifungashio vya bidhaa zenye chapa za kahawa na majani ya chai. Pia imewakamata watu saba, wawili kati yao wana asili ya Asia wanaodaiwa kuwa ni miongoni mwa […]

FEATURE
on Dec 27, 2023
285 views 45 secs

Tunakaribia kuumaliza mwaka huu na kuingia mwaka mpya 2024. Mwaka huu ulikuwa na mipango na mawazo mazuri mengi.Yako ambayo uliyafanyia kazi na ambayo hujayafanyia kazi. Kila mwaka lazima ufanye kitu cha ushindi, usiache mwaka uishe bila kupata kitu cha ushindi. “Kila mwaka unaopita ambao hujaharibu moja ya mawazo yako pendwa ni mwaka ambao umeupoteza” Kama […]

FEATURE
on Dec 27, 2023
377 views 17 secs

Vita vya Israel na wapiganaji wa Hamas huko Gaza vitaendelea kwa “miezi mingi zaidi”, mkuu wa jeshi la Israel amesema. “Hakuna suluhu za kichawi,” Herzi Halevi aliwaambia waandishi wa habari. Siku ya Jumatatu Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu alionya kwamba operesheni “haijakaribia kuisha”. Israel inasema ilipiga zaidi ya maeneo 100 siku ya Jumanne. Inaripotiwa kuendeleza operesheni […]

FEATURE
on Dec 27, 2023
339 views 24 secs

Wizara ya afya ya Gaza inayosimamiwa na Hamas imesema takribani watu 241 waliuawa katika kipindi cha saa 24 zilizopita, huku operesheni ya kijeshi ya Israel ikiendelea katika eneo hilo. Rais wa Palestina Mahmoud Abbas amevitaja vita hivyo kuwa ni uhalifu mkubwa dhidi ya watu wake. Mkuu wa jeshi la Israel Herzi Halevi alisema mzozo na […]

FEATURE
on Dec 27, 2023
380 views 17 secs

Israel imetoa tahadhari kwa raia wake nchini India baada ya mlipuko karibu na ubalozi wa nchi hiyo huko Delhi. Mlipuko huo ulifanyika Jumanne jioni katika eneo la kidiplomasia la mji mkuu wa Chanakyapuri. Hakuna mtu aliyejeruhiwa, lakini polisi walisema walipata vipande kutoka mahali hapo. Uchunguzi unaendelea. Israel imewataka raia wake kuepuka maeneo yenye watu wengi […]