Klabu ya Simba imefikia makubaliano ya pande zote mbili ya kuvunja mkataba na Kocha Mkuu wa kikosi cha kwanza Roberto Oliveira Goncalves Do Carmo (Robertinho) pamoja na kusitisha mkataba wa Kocha wa Viungo Corneille Hategekimana Simba imesema katika kipindi cha mpito kikosi kitakuwa chini ya Kocha Daniel Cadena akisaidiwa na Selemani Matola huku mchakato wa […]
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko leo Novemba 06, 2023 ameongoza Viongozi mbalimbali wa Serikali katika mazishi ya Mzee Issa Nangalapa ambaye ni kaka wa Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, Wilaya ya Ruangwa, Lindi. Akizungumza katika ibada ya mazishi Dkt. Biteko amempa pole Mheshimiwa Majaliwa na kwamba ujio wa viongozi […]
Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Silvestry Koka amempongeza kwa dhati Rais wa awamu ya sita Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kukubali kutoa kiasi shilingi milioni 252 kwa ajili ya ukarabati wa daraja la mto Mpiji ili liweze kuwasaidia wananchi wa kata ya pangani kuvuka kwa urahisi hasa katika kipindi hiki cha mvua. Koka ametoa pongezi […]
Akizungumza baada ya timu yake kufungwa magoli 5-1 katika mchezo dhidi ya Yanga, Kocha wa Simba, Roberto Oliveira โRobertinhoโ amesema kipindi cha pili wachezaji wake walipoteza umakini na ndio maana wakaruhusu magoli mengi Amesema โMagoli mawili tuliyofungwa kipindi cha pili wachezaji wetu (Simba) walizubaa na kupoteza umakini, walifikiri kuna faulo wenzetu wakaendelea kucheza na wakafunga. […]
Wananchi wametakiwa kuwapa ushirikiano Askari wa Wanyamapori Vijijini (VGS) ili waweze kutekeleza Majukumu yao vizuri ya ulinzi wa Maliasili pamoja na kuwalinda wanavijiji dhidi ya Wanyamapori wakali na waharibifu. Wito huo umetolewa na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Kamishna Benedict Wakulyamba kwenye ziara yake ya kukagua utekelezaji wa mradi wa Kuboresha Usimamizi […]
Wananchi wa Kijiji cha Chabula, Kata ya Nyanguge Wilayani Magu wameishukuru Serikali kupitia Wizara ya Maji kwa kuwajengea mradi wa maji ambao umekuwa na msaada mkubwa katika maisha yao. Wametoa shukrani hizo kwa nyakati tofauti mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. CPA. Amos Makalla wakati wa ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo […]
Yaeleza hatua ilizochukua kwa wafanyakazi na Kampuni zilizosababisha hasara Dodoma Serikali imeeleza hatua stahiki zilizochukuliwa kufuatia hasara iliyojitokeza kwa Serikali kupitia Kampuni ya mafuta ya TANOIL ikiwemo hatua ya kuwasimamisha kazi wafanyakazi wanne wa TANOIL. Hatua hizo zimeelezwa na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga kwa niaba ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa […]
SERIKALI imeombwa kupeleka huduma ya mawasiliano ya simu za kiganjani katika kijiji cha Epanko Halmashauri ya Mji Mahenge wilaya ya ulanga Mkoani Morogoro ili kurahisha mawasiliano katika uendeshaji shughuli za uchimbaji madini ya vito (Spinel) katika kijiji hicho. Mbali na hilo pia imeombwa kuboresha huduma ya upatikanaji wa nishati ya umeme wa uhakika katika maeneo […]
MAMLAKA ya Dawa na Vifaa Tiba Nchini (TMDA) inaendesha mafunzo ya siku tatu Jijini Dar es Salaam ya kufanya tathmini ya udhibiti wa vifaa tiba vya Wamama, Watoto wachanga na Watoto kwa wataalam wa vifaa tiba kutoka Mamlaka za udhibiti za nchi 11 za Afrika. Kongamano hilo ni la kwanza Barani Afrika ambapo mafunzo hayo […]
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Wakili Amon Mpanju amewataka Wakuu wa vyuo Vya Elimu ya Juu na Kati kuteua Waratibu Dawati la Jinsia waadilifu, katika kutatua changamoto za ukatili wa kijinsia vyuoni. Mpanju amesema hayo wakati akifungua mafunzo ya namna bora ya uanzishaji wa madawati ya jinsia […]