40 views 2 mins 0 comments

DSE NA FINTECH WASAINI MAKUBALIANO YA KUKUZA MATUMIZI YA SULUHISHO ZA KITEKNOLIJIA NA USHIRIKIANO WA MASOKO

In BIASHARA
April 17, 2025

Na Madina Mohammed DAR ES SALAAM WAMACHINGA

Soko la Hisa Dar es salaam  DSE limesiani Makubaliano (MOU) na jumiya ya  Fintech society Tanzania yenye lenga la kukuza matumizi ya suluhisho za kiteknolojia katika ushirikinw masoko ya mitaji na kuwawezesha  watanzania kupata elimu ya Fedha.

Akizungumza na waandishi wa Habari leo Aprili 17 wakati wakusaini Makubaliano hayo , Mtendaji Mkuu wa Soko  la Hisa Bw. Peter Nalitolela  Amesema ushirikiano huo utaangiza katika maeneo mbalimbali ikwemo kusaidia mabadiliko ya kidigitali katika huduma za kifedha na kujenga uwezo kqa vijana na wataalam sekta ya fedha.




“Teknolojia ya Fedha ni teknolojia ambayo imekuwa Kwa Kasi sana Kwa kujitika Kwa Kupitia mitandao ya simu kuwawezesha wadau kupata huduma za kifedha kama vile kufanya malipo kuwekeza kutuma pesa sehemu mbalimbali na kuhifadhi kuunga mkono juhudi za kiserikali za uelimishaji wa kifedha teknohama ni sehemu muhimu sana tunapunguza usumbufu” amesema

Ameongeza kuwa  Wao kama soko la Hisa wamekuwa wanafanya jitihada hizo binafsi kupitia mtandao wao wa uwekezaji kwa kushirikiana na wadau qa fedha na kukuza juhudi za kuwafikia wananchi katika kuwekeza soko la Hisa




Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa  Fintech society Tanzania Dr Deniss Mwighusa amesema wamefanya   tafiti mbalimbali Kwenye  maswala ya teknolojia ya Fedha ni kitu ambacho Kwa kiasi kikubwa sana kinakuwa


” Tunajaribu kuangalia wapi  na tunahitaji kufanya nini na  tumefanya utafiti Katika maswala ya teknolojia ya Fedha basi Ili kuweza kufanikisha tunafanya vizuri huku tukiangazia Maswala ya Mafunzo na Moja ya maeneo ya Siri sana ambayo tunaelekea kufanya Katika mambo ambayo tutafanya  na DSE ” amesema  Mwighusa

/ Published posts: 1932

Ukurusa rasmi wa gazeti la Wamachinga. #sautiyawanyonge

Twitter
Youtube
Instagram