51 views 4 mins 0 comments

RAIS SAMIA MGENI RASMI TUZO ZA KIMATAIFA ZA KUHIFADHI QURAAN

In KITAIFA
January 31, 2025

Na Mwandishi Wetu WAMACHINGA


RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Tuzo za  za Kimataifa ya Kuhifadhi Quraan yatakayofanyika Aprili 23 katika Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.


Aidha Taifa la Saudi Arabia, limetangaza neema katika mashindano hayo ikiwa ni pamoja na  kumleta mmoja wa maimamu wakubwa wa msikiti mtakatifu wa Macca nchini  humo na  kutoa tiketi za hija  kwa watu watano  ambao watakuwa ni wageni wa Mfalme wa   taifa hilo.


Akizungumza  na waandishi wa habari, Dar es Salaam, jana,Mwenyekiti wa Taasisi ya Kuhifadhisha Quraan Tanzania ambao ni wandaaji wa tukio hilo, Sheikh Othuman Kapolo, alisema, washiriki  katika mashindano hayo ni  25 kutoka mabara yote matano duniani.


“Awamu hii tutafanyia  tukio hili katika Uwanja wa Benjamin Mkapa. Panapo maajaliwa mgeni  Rasmi  anatarajia kuwa Rais Dk. Samia,”alisema.


Alieleza, mashindano hayo awamu hii yatashirikisha  makundi mawili ya  watoto  na vijana  wa umri wa miaka kuanzia 17 na 25.


“Tunawashukuru wenzetu wa  Saudi Arabia wamekubari  kushiriki kikamilifu katika maandalizi na kufanikisha tukio lote  la utoaji wa tuzo hizi. Wameahidi watatoa tiketi tano  kwa wananchi watakaofika katika Uwanja wa Mkapa kwaajili ya kwenda Hija nchini  humo,”alisema  Sheikh Kapolo.


Alisema licha ya tiketi hizo pia kutakuwa na zawadi mbalimbali  kwa wananchi watakaohudhuria  zikiwemo  simu na pikipiki, hivyo kuwahimiza wananchi kuhudhuria kwa wingi  kwani  hakutakuwa na kiingilio.


Alisema kwa washindi watakaoshindanishwa  katika  kuhifadhi Quraan tukufu  watakabidhiwa tuzo  za kimataifa  ambapo pia tuzo mbalimbali za kitaifa zitatolewa.


Alisema ujumbe wa utoaji wa Tuzo za Kimataifa za Quraan mwaka huu  usema Quraan ni amani.


“Pia ujumbe huu umezingatia mwaka huu ni mwaka wa Uchaguzi Mkuu, hivyo amani  tuliyonayo tunatakiwa kuilinda na Quraan ni amani,”alisema Sheikh Kapolo.
Awali Balozi wa Saudi Arabia hapa nchini , Yahya Ahmed Okeish, alisema   tuzo za kimataifa za Quraan tukufu  kama mbegu iliyopandwa na imechipua  kwa watanzania.


” Fahari ya Mola  katika Quraan ni kwamba yeye ndiye aliyeshusha Quraan na yeye ndiye  anayeitunza Quraan ispotee. Lakini  cha kushukuru katika maeneo mbalimbali duniani kuna ambao wamejitolea  kuisimamia  kupitia  vijana mbalimbali kwa kuwahifadhisha.

Miongoni mwao ni  Sheikh Othuman Kapolo,” alisema Balozi Okeish.
Alisema, mwongoni mwa bipaumbele  vya Mfalme wa SaudiArabia ni kuwahudumia watu wa Quraan.


Katika Mji Mtakatifu wa Madina kuna kiwanda kinacho chapisha  misahafu katika mifumo mbalimbali, ikiwemo ya kusoma, sauti na kwa wasioona   hivyo taifa hilo linanafasi kubwa ya kuhakikisha usomaji wa Quraan unasonga mbele.
Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega ambaye ni Mbunge wa Mkuranga, yalipo makao makuu ya Taasisi ya Kuhifadhisha Quraan Tukufu Tanzania, aliwataka wananchi kuhidhuria kwa wingi katika masgindano hayo muhimu.


Ulega alisema ujumbe wa mwaka huu wa  Quraan ni amani  ambao ni  muhimu  hasa wakati huu  ambapo taifa linaelekea katika uchaguzi mkuu.


Alisema Rais Dk. Samia, amelekeza wasaidizi wake yapofika mambo mema  hasa ya kidini  ni kuyapa kipaumbele.
Awali akizungumza kwa niaba ya Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Abubakar Zubeir, Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Walid Alhad, aliwataka wananchi kujitokeza kwa wingi kuhudhuria tukio hilo muhimu.


“Jambo hili lionekane linasimasishwa kwa hadhi ya Rais  na hadhi ya Quraan,”alisema Sheikh Alhad.

/ Published posts: 1749

Ukurusa rasmi wa gazeti la Wamachinga. #sautiyawanyonge

Twitter
Youtube
Instagram