15 views 2 mins 0 comments

MHE.CHANA AZINDUA ZAHANATI YA IVILINGIKE-MAKETE

In KITAIFA
September 16, 2024

Na Mwandishi Wetu WAMACHINGA

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Njombe na Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Balozi, Dkt. Pindi Chana (Mb) amezindua rasmi zahanati ya Ivilikinge iliyopo Wilayani Makete Mkoani Njombe sambamba na kukabidhi vifaa mbalimbali vya hospitali vilivyotolewa na Benki ya NMB.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi huo, leo Septemba 16,2024, Mhe. Chana amesema uwepo  wa zahanati hiyo ni miongoni mwa vipaumbele vya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan vya kuhakikisha huduma za afya zinawafikia  wananchi mpaka vijijini.

” Hizi ni baadhi ya huduma tulizoahidi kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi hivyo tunapochagua viongozi tuchague ambao watatuletea maendeleo” amesisitiza Mhe. Chana.

Amesema kuwa kupitia zahanati hiyo wananchi wa Isapulano na vijiji vya jirani watapata huduma  bora za afya na kuwaomba wananchi hao kuhakikisha wanaitumia ipasavyo zahanati hiyo.

Naye, Kaimu Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Nyanda za Juu, Willy Mponzi amesema kwa kuzingatia  juhudi za Rais katika kusimamia upatikanaji wa huduma bora za afya mijni na vijijini, changamoto  za Sekta ya Afya  ni kipaumbele kwa Benki ya NMB kwa sababu afya ni kipaumbele kwa maendeleo ya Taifa lolote.

Kufuatia hatua hiyo,benki ya NMB inakabidhi vifaa mbalimbali vya hospitali kwa zahanati hiyo ikiwemo Vitanda vya kujifungulia (2),Vitanda vya uchunguzi (2),vitanda vya hospitali (5),Magodoro (5),folding screen (4),folding stretcher (2),delivery kit (5),drip stend(5), mashuka 50 na viti vyenye magurudumu (3) vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 9.

Awali, akiwasilisha taarifa ya ujenzi wa mradi huo, Mganga Mkuu wa Zahanati ya Isapulano, Hassan Omar  alisema kuwa mradi huo umegharimu takribani milioni 146.1 ambayo inatokana na michango ya wananchi (milioni 26.5), Wadau wazawa (milioni 6.6, Mbunge wa Jimbo la Makete,Mhe. Festo Sanga (milioni 4) ,Diwani (laki 5 na elfu 30), Benki ya NMB Mabati (milioni 8.5) na Serikali (milioni 100).

Amefafanua kuwa lengo la mradi huo ni kuboresha upatikanaji wa huduma za afya kwa wananchi wa Ivilikinge na vijiji vya jirani, kupunguza umbali wa kufuata huduma kwa mama wajawazito, watoto na wazee.

/ Published posts: 1214

Ukurusa rasmi wa gazeti la Wamachinga. #sautiyawanyonge

Twitter
Youtube
Instagram