71 views 45 secs 0 comments

RC CHALAMILA AMEZIAGIZA MAMLAKA DAWASA,DART NA TARURA KUBORESHA MIUNDOMBINU GEREZANI

In KITAIFA
May 29, 2024

Na Madina Mohammed DAR ES SALAAM WAMACHINGA

Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam ALBERT CHALAMILA ameziagiza mamlaka za Usimamizi wa maji safi DAWASA, DART pamoja na TARURA  kuboresha miundombinu ya maji taka pamoja na ujenzi ujenzi wa barabara katika mtaa wa lindi kata ya gerezani wilaya ilala jijini Dar es salaam


Ameyasema hayo Leo Tarehe 29 Mei 2024 mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Albert Chalamila katika ziara maalumu ya ukaguzi wa ujenzi wa miundombinu mbalimbali katika jiji la Dar es salaam


Ziara hiyo ya kusikiliza kero za wananchi inamfikisha  mkuu wa mkoa wa Dar es salaam  ALBERT CHALAMILA   katika mtaa wa lindi  kata gerezani jijini dsm  kushuhudia changamoto za miundombinu ya barabara pamoja na mitalo ya kupitisha maji taka


Ambapo anasema changamoto hiyo natokana na ujenzi mbovu wa miundombinu hiyo Kutokana na uzembe wa usimamizi  wa ujenzi wa miundombinu hiyo mkuu wa mkoa anatoa agizo kwa wasimamizi  hao

Chalamila Anaenda mbali zaidi na kuziagiza balozi mbalimbali nchini pamoja  jengo la PSSF  lililoko posta jijini DSM kuondoa mifumo ya kupitisha  maji taka  katika njia za maji safi.

Ubovu wa miundombinu ya barabara, ujenzi holela wa makazi pamoja na ujenzi mbovu wa mitalo  ya  kupitisha maji taka unatajwa kuwa ni wimbo wa taifa ambapo kwa kiasi kikubwa  maeneo mengi nchini kukumbwa na mafuriko

/ Published posts: 1214

Ukurusa rasmi wa gazeti la Wamachinga. #sautiyawanyonge

Twitter
Youtube
Instagram