
Na Mwandishi Wetu WAMACHINGA
Aliyekuwa Rais wa Uganda marehemu Idi Amin alitaka kubadilisha jina la Uganda kuwa IDI. Kila mtu katika baraza la mawaziri alikubali. Sababu ni kuwa ‘Walimwogopa’. *Lakini kulikuwa na mtu mmoja, Malyamungu.* Akamwambia Amin “Mhe Rais unaijua nchi inayoitwa Cyprus?” Basi Amin akamuuliza “Hivyo Cyprus ina uhusiano gani na Mabadiliko ya Uganda, Kuwa IDI?” Malyamungu akamjibu “raia wa Cyprus huitwa cypriots, *Ikiwa tutabadilisha jina la Uganda kuwa IDI, hivyo sisi Waganda tutaitwa idiots, na ulimwengu utatuita IDIOTS [ Wapuuzi ], ilhali hatuko hivyo.*
Hivyo Idi Amin alimwangalia na kusema *”Wewe na mimi, ndio wanaume wenye akili zaidi katika baraza zima la mawaziri.* Na jina la nchi litabaki kuwa ni Uganda”. Na kwa hivyo, lilibaki hadi leo!
Kweli ilikuwa ‘Sauti Moja’ ya Malyamungu lakini ilisimamisha mchakato mzima. *Ukimya wa watu wema hufanya uovu kutawala,* nyumba ya jirani ikiwaka moto hakika hauchukui jembe ukalime!
Tutafakari katika maneno haya….