19 views 2 mins 0 comments

MIGOGORO YA WAMACHINGA NA SERIKALI YAFIKIA KIKOMO

In BIASHARA
September 11, 2024

Na Madina Mohammed DAR ES SALAAM WAMACHINGA

Viongozi wa Shirikisho la  Umoja wa wafanya biashara ndogondogo (Machinga)kutoka katika Mikoa  20 ya Tanzania bara wamekutana leo 11Septemba mwaka huu  jijini Dar es Salaam ambapo wamekuwa na maazimio mbalimbali ya kuimarisha umoja wa shirikisho hilo.



Akizungumza katika mkutano huo Uliofanyika JM Hotel Mwenyekiti wa Muda wa shirikisho la Wamachinga  Steven Lusinde amesema lengo la mkutano huo nikuweka wazi maazimio ya wamachinga wote nchini ambapo lengo kuu likiwa ni kufanya marekebisho ya rasimu ya katiba ya wamachinga kwa mujibu wa maelekezo ya msaji wa vyama vya kiraia nchini, kuanzisha SACCOS za wamachinga  zitakazosajiliwa Nchi nzima na kutatua migogoro baina ya wamachinga na Serikali.



Katika hatua nyingine Lusinde kwa niaba ya wamachinga wote amemshkuru Rais Samia Suhulu kwa kujenga vituo vya biashara vya wamachinga  (Machinga Comprex) na kuongeza kuwa  wamachinga wanaunga mkono juhudi za serikali za kuleta maendeleo na kwamba wapo tayari kutoa ushirikiano kwa kulipa kodi ili kukuza uchumi.

Akizungumza katika kikao hicho Lusinde amesema kuanzishwa kwa SACCOS hizo kutaweka urahisi kwa wamachinga kupata fursa ya mikopo ambayo inatolewa na Rais Samia Suluhu Hassan na kwamba imekuwa vigumu kwao kupata mikopo hiyo inayopitia Halmashauri kutokana na kutokuwa na SACCOS na vikundi maalum.



“Tunatamani tuwe na elimu juu ya kitambulisho cha mjasiliamali tujue faida ya kuwa na kitambulisho ili tununue bila kusukumwa”ni ombi lililowasilishwa na mwenyekiti wa shirikisho Steve Lusinde mbele ya waandishi wa habari wakati akizungumza katika kikao cha viongozi wa Machinga 11 Septemba mwaka huu Jijini Dar es Salaam.

/ Published posts: 1214

Ukurusa rasmi wa gazeti la Wamachinga. #sautiyawanyonge

Twitter
Youtube
Instagram