29 views 0 secs 0 comments

TANAPA WAPOKEA CHETI USHIRIKI WA TAMASHA LA KIZIMKAZI

In KITAIFA
August 25, 2024

Na Mwandishi Wetu WAMACHINGA ZANZIBAR

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt Samia Suluhu Hassan amekabidhi cheti cha pongezi kwa ushiriki wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) kwenye tamasha la Kizimkazi Festival 2024 Hafla ya chakula cha usiku iliyofanyika Ikulu ndogo Kizimkazi Zanzibar.

Cheti hicho cha pongezi kimepokelewa kwa niaba ya Kamishna wa Uhifadhi wa TANAPA, Nassoro Juma Kuji, na Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi, Jully Bede Lyimo – Mkuu wa kitengo cha  Maendeleo ya Biashara pamoja na Afisa Uhifadhi Mwandamizi Amina R. Salum ambaye ni Afisa Utalii Hifadhi ya Taifa Ruaha.

TANAPA, kwa dhati na unyenyekevu mkubwa tumepokea na kuthamini heshima hii kubwa kutoka kwa Mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan.

/ Published posts: 1214

Ukurusa rasmi wa gazeti la Wamachinga. #sautiyawanyonge

Twitter
Youtube
Instagram