51 views 2 mins 0 comments

MAKAMU WA RAIS KAMALA HARRIS KUKAMILISHA MAKUBALIANO YA AMANI NI KULETA SULUHISHO YA VITGA VYA GAZA

In KIMATAIFA
July 26, 2024

Na Rachel Tungaraza

Makamu wa Rais wa Marekani, Kamala Harris, ameonesha mabadiliko katika sera za Marekani kuhusu Gaza. Katika mazungumzo yake na Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, Kamala Harris amesisitiza umuhimu wa kukamilisha makubaliano ya amani na kuleta suluhisho juu ya vita vya Gaza ambavyo vimesababisha hasara kubwa kubwa nchini humor na vifo vya watu wengi.

Kamala Harris alionyesha ishara hiyo waziwazi katika mazungumzo hayo, akiongeza kuwa ni wakati muafaka kumaliza vita vya Gaza ambavyo vimeleta mateso makubwa kwa raia. Alisema kuwa Marekani inataka kuona amani ya kudumu katika eneo hilo na itaendelea kushirikiana na pande zote ili kufikia lengo hilo.

Katika mazungumzo hayo, Kamala Harris alieleza kuwa vita vya Gaza vimeleta athari mbaya sana, ikiwa ni pamoja na vifo vya raia wasio na hatia na uharibifu wa miundombinu muhimu. Alisisitiza kuwa ni jukumu la viongozi wa pande zote mbili kutafuta suluhisho la kudumu na kuachana na ghasia ambazo hazileti manufaa yoyote kwa wananchi.

Aidha, Kamala Harris alimhakikishia Netanyahu kuwa Marekani iko tayari kusaidia katika mchakato wa amani na kwamba itaendelea kushirikiana na Israel pamoja na Palestina ili kufikia makubaliano yatakayodumisha amani na utulivu. Alisema kuwa ni muhimu kwa viongozi kuwa na nia ya kweli ya kutafuta amani na kuzingatia maslahi ya wananchi wao.

Mazungumzo hayo yalikuwa na lengo la kuimarisha juhudi za kimataifa za kumaliza mgogoro wa Gaza na kuleta amani katika Mashariki ya Kati. Kamala Harris alitoa wito kwa pande zote mbili kuonyesha nia yake   katika kutafuta amani na kushirikiana kwa karibu na jumuiya ya kimataifa ili kufikia malengo hayo.

Kamala Harris alisisitiza kuwa Marekani itaendelea kuwa mshirika wa karibu wa Israel na Palestina katika juhudi za kuleta amani na kuhakikisha kuwa vita vya Gaza vinakuwa historia. Alisema kuwa ni wakati wa viongozi kuonyesha uongozi wa kweli na kujitolea kwa dhati kwa ajili ya ustawi wa wananchi wao na amani ya kudumu.

/ Published posts: 1214

Ukurusa rasmi wa gazeti la Wamachinga. #sautiyawanyonge

Twitter
Youtube
Instagram