112 views 14 secs 0 comments

SAMAKI SAMAKI KUJA NA KAMPENI YA HATUSHIKIKI YENYE OFA KABAMBE

In BIASHARA, BURUDANI
June 10, 2024

Na Madina Mohammed DAR ES SALAAM WAMACHINGA

Katika kuhakikisha burudani hazipoi na kuwafikia watanzania Hatushikiki imekuja na kuzama kwa jua ili kukuza sekta ya burudani na kuwafanya wasanii kutoa burudani ya aina yake.

Akizungumza jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mtendajiย  wa Kalito’s Way Group of Companies, Carlos Kalito, amesema kuwa wana sheherekea mafanikio ya biashara yake ya migahawa nchini Tanzania yatokanayo na ubunifu kwa kutoa nafasi kwa wasanii mbalimbali

.

Kampuni hiyo, ambayo inajumuisha migahawa ya Samaki Samaki, Kuku Kuku, na maarufu Wavuvi Kempu, inaajiri jumla ya Watanzania 500 kwa kuweza kutoa burudani za usiku.

“Maadhimisho ya miaka 17, yaliyopewa jina la “Hatushkiki Tunaua Kila Siku,” Kalito alisisitiza mazingira mazuri ya uwekezaji nchini Tanzania kama sababu kuu ya mafanikio yao.



“Nina fahari kuchangia soko ajira kwa wasanii mbalimbali kutoa burudani licha ya changamoto, hasa ushindani wa soko. Tuna watu wabunifu na wavumbuzi ambao wametusaidia kufikia mafanikio haya, na tunaendelea kusonga mbele.

/ Published posts: 1215

Ukurusa rasmi wa gazeti la Wamachinga. #sautiyawanyonge

Twitter
Youtube
Instagram