108 views 11 secs 0 comments

SILINDE:TUNAONYESHA UMMA MABADILIKO CHANYA AMBAYO WIZARA IMEKUWA IKIYAFANYA KATIKA SEKTA YA KILIMO

In BIASHARA, KITAIFA
May 03, 2024

JIJINI DODOMA

Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. David Silinde (Mb) amesema lengo la Wizara kuweka maonyesho katika viwanja vya Bunge ni kuonesha Umma mabadiliko chanya ambayo  Wizara imekuwa ikiyafanya katika Sekta ya Kilimo kuanzia katika ngazi ya tafiti mpaka katika ngazi ya uwekezaji ya kuongeza thamani ya mazao.


“Tunaonesha watu namna ambavyo tunaendesha Sekta ya Kilimo Kidigitali yaani kwa kutumia vifaa vya kisayansi na teknolojia ikiwemo na namna ya kukabiliana na magonjwa mbalimbali, wadudu waaribifu wakiwemo ndege na viuatilifu, kuangalia matumizi sahihi ya mbolea” ameeleza Mhe Silinde.

“Sisi wizara ya kilimo tunaamini kilimo katika njia ya kutumia sekta ya umwagiliaji (irrigation skims pamoja na mabwawa) tunaamini hii ndio inaweza kubadiloisha sekta ya uchumi” ameongezea Mhe Silinde.

Maonyesho hayo yamehudhuriwa na Wabunge mbalimbali pamoja na viongozi mbalimbali wakiwemo Mawaziri na Manaibu Waziri wa Wizara mbalimbali pamoja na Wakuu wa Taasisi mbalimbali za Umma.

/ Published posts: 1215

Ukurusa rasmi wa gazeti la Wamachinga. #sautiyawanyonge

Twitter
Youtube
Instagram