138 views 47 secs 0 comments

BRT,FLY OVERS NA BARABARA KUPUNGUZA MSONGAMANO WA MAGARI KATIKA MIJINA MAJIJI YATATEKELEZWA

In KITAIFA
April 05, 2024

DODOMA

Waziri wa Ujenzi Innocent Bashungwa amesema, Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea na miradi mbalimbali ya kupunguza msongamano wa  magari katika Miji na Majiji kwa kujenga barabara za juu (Fly Overs) kwenye Makutano ya barabara, Ujenzi wa Miundombinu ya Mabasi yaendayo haraka (BRT).

Bashungwa ameeleza hayo jijini Dodoma katika hafla ya kuangazia Mafanikio ya Miaka Mitatu Madarakani ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Ametaja majiji ambayo miradi hiyo ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji ikiwemo jiji la Dar es Salaam, Dodoma, Mwanza, Mbeya na Arusha.

/ Published posts: 1215

Ukurusa rasmi wa gazeti la Wamachinga. #sautiyawanyonge

Twitter
Youtube
Instagram