191 views 17 secs 0 comments

Israel yatoa tahadhari baada ya mlipuko karibu na ubalozi nchini India

In KIMATAIFA
December 27, 2023

Israel imetoa tahadhari kwa raia wake nchini India baada ya mlipuko karibu na ubalozi wa nchi hiyo huko Delhi.

Mlipuko huo ulifanyika Jumanne jioni katika eneo la kidiplomasia la mji mkuu wa Chanakyapuri.

Hakuna mtu aliyejeruhiwa, lakini polisi walisema walipata vipande kutoka mahali hapo. Uchunguzi unaendelea.

Israel imewataka raia wake kuepuka maeneo yenye watu wengi kama vile maduka makubwa na masoko, na matukio makubwa.

Iliongeza kuwa “inawezekana” mlipuko huo ulikuwa “shambulio” na kulikuwa na “hofu ya kujirudia kwa matukio”. Katika ujumbe wa hadharani siku ya Jumanne, Makao Makuu ya Usalama wa Taifa (NSH) pia iliwaonya Waisraeli wanaokaa India hasa mjini Delhi haswa kuwa macho, waepuke kuonesha “ishara za Israeli” hadharani na wasichapishe maelezo ya safari au picha zao kwenye mitandao ya kijamii.

Mapema mwezi huu, NSH ilionya Waisraeli kufikiria upya safari zao zote nje ya nchi na kutoa wito kwa wale wanaohitaji kusafiri ng’ambo kuepuka utambulisho wao wa Kiyahudi wakati wa vita vinavyoendelea huko Gaza.

/ Published posts: 1209

Ukurusa rasmi wa gazeti la Wamachinga. #sautiyawanyonge

Twitter
Youtube
Instagram