139 views 24 secs 0 comments

MUIMBAJI JOYCE MWAIKOFU AMEWAOMBA SERIKALI KUTOA ELIMU KWA WAIMBAJI AMBAO HAWAJUI BASATA NA COSOTA

In BURUDANI
October 23, 2023

Muimbaji wa Gospel Joyce Mwaikofu Ameiomba serikali kutoa Elimu Kwa wasanii na waimbaji ambao hawajui BASATA na Cosota Ili kuweza kutoa Elimu Kwa waimbaji hao

Amesema fursa nyingi huwa zinakuja za nje na ndani Kupitia serikali na serikali haiwezi kutoa msaada Kwa mtu mmoja wanaitaji waunde vikundi au vyama vya waimbaji Ili pindi fursa hizo zinapokuja ziwafikie Kwa wote na amesema waimbaji wa injili wapo nyuma sana na hawaelewi

Akizungumza wakati Akiitambulisha Nyimbo yake ya Nitaifuta Machozi Hapo Jana Katika kumbi za center point Mwaikofu amesema Mziki ni TIba kwani Kuna watu wanapitia matatizo ya kisononi na magonjwa mbalimbali yanashuka Kwa Kupitia mziki Unaweza kujitibu

Aidha Mwaikofu amesema Kwa Sasa Kuna changamoto Katika YouTube amesema kunaitaji uwekezaji wa nguvu na Ili kuweza kujulikana na kupata promo unaitaji umpate Mtu ambae anaeijua IT Ili kuweza kuweka mitandao Yao vizuri na changamoto ya watu wengi hawana kipato

Hata hivyo Mwaikofu Ameishukuru serikali Kupitia waziri na Naibu waziri wa Utamaduni sanaa na michezo kuona changamoto zao wanazozipitia Katika uimbaji wao

Madina Mohammed

/ Published posts: 1215

Ukurusa rasmi wa gazeti la Wamachinga. #sautiyawanyonge

Twitter
Youtube
Instagram