
Wanajeshi wamehamishwa kutoka kambi ya jeshi kaskazini mwa Mali kufuatia shambulio la watu wenye silaha, jeshi la taifa hilo limesema.
Wanajeshi wa Mali waliwakabili washambuliaji huko Acharane, eneo karibu na mji wa kale wa Timbuktu, taarifa ilisema.
Bado haijabainika iwapo watu hao wenye silaha walikuwa wanamgambo wa Kiislamu au waasi wa Tuareg.
Makundi yote mawili yameongeza mashambulizi yao katika wiki za hivi karibuni – wakati ambapo walinda amani wa Umoja wa Mataifa wanaondoka nchini humo baada ya kuamriwa kuondoka na watawala wa kijeshi wa Mali.