168 views 30 secs 0 comments

ALIEKUWA MWENYEKITI TUME YA UCHAGUZI ZANZIBAR ZEC AFARIKI DUNIA

In KITAIFA
July 18, 2023

MWENYEKITI wa zamani wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) Jecha Salum amefariki dunia leo.

Taarifa zinaeleza Jecha Salum amefariki akiwa katika Hospitali ya Lugalo Dar es Salaam.

Maziko yanatarajiwa kufanyika Mkoa wa Kaskazini Unguja Visiwani Zanzibar.

Ikumbukwe mwenyekiti huyo aliwahi kufuta matokeo ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2015. Mwaka 2020, Jecha alichukua fomu ya kugombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM).

/ Published posts: 1214

Ukurusa rasmi wa gazeti la Wamachinga. #sautiyawanyonge

Twitter
Youtube
Instagram