241 views 2 mins 0 comments

STEVE NYERERE NA YOGE KUSHIRIKIANA KUWASAIDIA WATOTO MADAFTARI

In KITAIFA
July 04, 2023

Msanii Steve Nyerere Kwa kushirikiana na shirika la yoge wameanda mpango wa kuwasaidia watoto wasioweza kujikimu Katika vifaa vya masomo Yao na wazazi ambao wasioweza kufanikisha Maendeleo ya watoto wao.

Yoge imeandaa mpango huo Kwa kufanikisha watoto wanasoma vizuri na kupata vitendea kazi kama madaftar na kuazisha kampeni ya mama ongea na mwanao

“Kuna watoto hawaendi darasani Kwa sababu Hana daftari wakati Kuna nafasi kama mzazi kukamilisha malezi ya mtoto ila Kuna mzazi amerudi na amelewa ila sisi Sasa tumeamua tuonyeshe mwanga,Mwanga ule ni mwanga wa kuhakikisha tunaendelea kuwa mfano WA kuigwa”. Alisema Nyerere

Aidha wanakampuni makubwa taasisi mbalimbali sio tu kudhamini vitu vya starehe ila ufike Muda tunauwezo wa kudhamini tukawarudisha watoto mashuleni tukawajenga wakati wa elimu bola na Wenye tabasamu na Wenye uhakika.

“tunamsaidiaje mzazi tukimsaidia mzazi daftari na viatu serikali yeye inawasaidia mzazi kutolipa ada Kwa hiyo tunajenga taifa la kesho na kesho kutwa la watoto Wenye kujitambia na kuwa na elimu ya kutosha”. Ameongeza Nyerere

Nyerere amemaliza Kwa kusema tukajenge misingi ya elimu na tujenge misingi ya kujikomboa na usijikomboe wewe mkomboe na mtoto WA jirani yako hivi tunaweza kuijenga nchi yetu.

Nae mkurugenzi wa yoge Rose chilonjaki amesema yoge Kama shirika Kwa Kasi yetu sisi shughuli zetu Cha kwanza ni kuwa na elimu pili tuwe na usawa WA Jinsia na Maendeleo ya jamii tatu kuwa na demokrasia na nne mabadiliko ya jamii Kwa utafiti yetu ndogo ambayo tuliyoifanya tuliona kama ni vyema tuanze Katika jamii.

“Katika kutatua changamoto za uhaba wa umakini Kwa watoto wetu Kwa wanafunzi wetu sio tu waliopo getini na hata wale waliokuwa nje ya geti lakini tumijikwamua zaidina kupitia mradi huo rasmi kampeni ya daftari ya mama tunaamini tunaimani kuunga mkono Kwa kushikwa na wadau wa Maendeleo na wadau wa elimu na wadau Wenye mapenzi wanaoenda kuijenga vizazi bola Cha badae Kwa ajili ya manufaa Kwa taifa Kwa ujumla”.Alisema Chilonjaki

Hata hivyo Amesisitiza tunaamini kwamba Leo ni mwanzo wa safari yetu tutagusa upande wa bala na upande wa Zanzibar ni matumaini yetu mwenyezimungu atatujaalia afya njema.

Madina Mohammed

/ Published posts: 1215

Ukurusa rasmi wa gazeti la Wamachinga. #sautiyawanyonge

Twitter
Youtube
Instagram